Thursday, February 26, 2009

KARIBUNI TENA WADAU

Habari za siku nyingi wadau wa blog hii maridhawa. Kwa vile tangu mwaka wa 2009 uanze hatujawasiliana kwa namna moja au nyingine ningependa kuwatakia HERI YA MWAKA MPYA WA 2009. Nasema karibuni tena kwani ni kipindi kirefu nilikuwa sipo hewani kuwapatia vitu vizuri kwa ajili ya kuilinda afya yako.

Nawaomba radhi wadau wenzangu kwani nilitoweka ghafla bila kuwapa taarifa yeyote huku wengine mkijiuliza mwaswali yasiyo na majibu juu ya uwepo wangu hapa duniani. Labda niwaondoe wasiwasi kuwa mie nipo salama salimini na afya isiyo na mgogoro. Isipokuwa mambo fulani yalinifanya nikae kando bila kutoa mada yeyote katika safu ya blog hii.
Kwa sasa nimerejea kwa kasi ile ile. Maana sipendi kuwaongopea eti kasi mpya kwani wengi wetu hatujui hiyo kasi mpya inakuwaje kwa sababu imeonekana kutuletea madhara badala ya furaha.
Wakati wowote kuanzia sasa wadau mtaanza tena kupata ile elimu juu ya afya zetu kwa kutumia mazao asilia kama ilivyokuwa awali. Tutakiane afya njema ili tuweze kutimiza malengo yetu.
KARIBUNI SANA

No comments: