
2flag.blogspot.com Thamini maisha yako.Jali afya yako.


Najua ni vigumu kwa watu kufuata mpangilio huu. Lakini kama umedhamiria kuilinda afya yako unaweza na tena vyakula hivyo ni rahisi kuvipata katika masoko yetu hapa nchini TZ tofauti na wenzetu kule majuu.
Aidha niliposema kula kulingana na mahitaji ya mwili wako, unapaswa kujua wewe mwenyewe unafanya shughuli gani. Kwasababu, mahitaji ya miili yanatofautiana kulingana na aina ya shughuli au kazi ya mtu husika. Kwa mfano watu wanaofanya kazi maofisini na walimu wanahitaji kiasi kidogo cha chakula; kwa wanafunzi na wafanyabiashara na wachuuzi pamoja na watumishi wa kazi za ndani wanahitaji nyongeza kidogo tofauti na mtu wa ofisini; mafundi kama seremala, umeme, watumishi wa nyumbani wanaofanya kazi kama za kulisha mifugo na nyingine ngumu wanahitaji chakula cha kutosha; na wafanyakazi wa ujenzi kama wabeba zege, ujenzi wa barabara, migodini, wanariadha na wengine wa aina hiyo wanahitaji chakula kingi ili kutosheleza mahitaji ya miili yao kwani wao wanatumia calories nyingi. Hivyo ni vema ukazingatia hilo ili usije kula chakula zaidi ya mahitaji ya mwili wako na matokeo yake ni unene unaoweza kukusababishia matatizo au hata usipokuwa mnene unaweza kujikuta unapata kisukari kinyume na matarajio yako.
Kwa maelezo hayo nadhani nitakuwa nimejibu baadhi ya maswali ya wasomaji waliotaka kujua watakula nini, kwa kiasi na kiwango gani na wakati gani. Kumbuka, hapo baadaye nitakupa jinsi unavyotakiwa kupangilia milo yako kwa siku. Kama una maswali zaidi usisite kuuliza.
Asante kwa ushirikiano wenu na karibu tena.
Je, unafahamu kuwa watu tulio wengi tunachimbia makaburi yetu wenyewe kwa kutumia mikono, vijiko, visu na uma? Ni kwa nini nasema hivyo, kwasababu watu wengi tunapenda kula kila kitu kizuri tunachokiona kwa macho yetu na chenye ladha ulimini bila kujali athari za chakula chenyewe katika miili yetu. Tunakula vyakula vyenye sukari nyingi, mahanjumati yaliyokaangizwa kwa mafuta tusiyoyajua vizuri, chumvi nyingi ili tufurahishe ndimi zetu na vingine vingi vya namna hiyo kama wale wenzangu na mimi tunaopenda kwenda kujipumzisha ifikapo jioni au weekend katika maeneo fulani ya vimiminika huku tukipata nyama choma au kitimoto kwa wale walioamua kufumba macho. 

2FLAG

Kumbukeni unapoandaa vitu hivyo hapo juu ni lazima uzingatie usafi ukianzia wewe mwenyewe, vyombo utakavyotumia pamoja na matunda, siyo lazima upate matunda yote ili kukamilisha mchanganyiko ulioelezewa hapo juu, bali unaweza kuchukua baadhi kutegemeana na uwezo wako ili mradi tunda la msingi kama avocado lipo kwenye mchanganyiko wako. Matunda haya yapo karibu kila kona za mitaa ya Darisalama kwa wale waliopo jiji hilo, pia yanapatikana baadhi ya mikoa hapa nchini, hivyo siyo mpaka ushauriwe na daktari ndipo ule matunda, anza sasa kula matunda, japo moja kwa siku si haba.
Kwa wale watakaohitaji kujua maandalizi na matumizi ya avocado kwa ajili ya kutunza nywele au ngozi wanaweza kuwasiliana nami kupitia email zifuatazo: larkado@gmail.com au leofiderk@yahoo.com
Asante.
2FLAG


