Saturday, August 23, 2008

AVOCADO NA FAIDA ZAKE


Leo napenda niendeleze mada ya tunda la avocado pamoja na faida zake. Kabla ya kuongelea faida zake ningependa nielezee kwanza vitu ama virutubisho vinavyopatikana ndani ya tunda hilo. Vitu hivyo ni kama ifuatavyo;


MAJI: tunda hili lina kiasi kidogo cha maji tofauti na matunda mengine tuliyozoea kula.

MAFUTA: avocado lina kiwango kikubwa cha mafuta na ndani ya kiasi hicho cha mafuta kuna tindikali (acid) mbalimbali zinazosaidia kukinga na kutibu maradhi katika mwili.

PROTINI: tunda hili pia lina kiwango cha juu cha protini kutegemeana na aina ya tunda lenyewe. Ndani ya protini pia kuna tindikali (acid) aina ya amino.

VITAMINI "E": inadaiwa kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama, hata mayai hayana kiwango kikubwa ukilinganisha na tunda la avocado.

VITAMINI "B6": Nayo inapatikana kwa wingi.

MADINI YA CHUMA (Iron): Pia yapo kwa wingi.


Baada ya kuvielezea baadhi ya virutubisho vinavyopatikana katika tunda hili, sasa tuangalie faida zinazotokana ama kwa kula au kutumia tunda la avocado au matumizi ya mmea wenyewe. Kwanza kabisa ningependa ujue kwamba majani ya mti wa avocado pamoja na magamba ya mti wake yakitengenezwa vizuri yanatumika kutibu maradhi ya kuharisha, kuondoa gesi tumboni, kutuliza kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo. Dawa hii haishauriwi kutumiwa na akina mama wajawazito kwani inaweza kuwaletea matatizo yanayoweza kuharibu mimba. Aidha kwa wanawake ambao wameshindwa kuona siku zao kwa wakati, wanaweza kutumia mchanganyiko huo kwa nia njema ya kuwawezesha kuingia kwenye period.


Tunda la avocado ni chakula kizuri kwa watoto, pia lina madini ya potasiam (potassium) na vitamin B6 na E ambazo zinaweza kuleta nafuu kwa wale wenye matatizo ya stress, matatizo ya uzazi kama ugumba na uanithi. Tindikali aina ya oleic (oleic acid) iliyomo ndani ya tunda hili inasaidia kukinga dhidi ya magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa. Aidha tunda hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani tunda hili lina "fiber" ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya artery wanashauriwa kula tunda hili mara kwa mara. Tunda la avocado limethibitishwa kupunguza kwa kiwango kikubwa cholesterol kutoka kwenye damu hasa kwa wale wenzangu na mimi ambao ni wanene.


Matumizi ya nje ya mwili kwa tunda hili husaidia kulainisha ngozi na kuondoa makwinyanzi, kung`arisha na kulainisha nywele na kuzifanya zionekane nadhifu, linasaidia ukuaji wa nywele na pia kuimarisha na kuzuia kukatika kwa nywele.


Hakika tunda hili lina maana sana kwa maisha yetu ya kila siku na inashauriwa kula tunda hili mara kwa mara kutegemeana na uwezo wako kwani hautopoteza chochote utakapokula tunda hili. Mada ijayo nitakupa vidokezo vichache namna ya kuandaa tunda hili kabla ya kuliwa.


Endelea kuwa pamoja nami katika toleo lijalo.


2FLAG.

2 comments:

Anonymous said...

Is there any research made for your observation? Any way, your articles are good for our health.

Keep it up bro.

Anonymous said...

Hii ndio shule ya kweli..asante mdau kwa huu mchango wako..Gluv100