Thursday, September 18, 2008

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME (SEXUAL IMPOTENCE)

Hongera kwa saumu kwa wale waliofunga, na wale wenzangu na mie habari za siku tele. Ndugu zangu msidhani kama niliingia mitini bali dharura za kimaisha zilinizonga. Leo naomba nizungumzie kuhusu suala nyeti la upungufu wa nguvu za kiume na namna ambavyo mtu mwenye tatizo kama hili anaweza kutumia ushauri wangu ili kurejesha heshima yake katika kufanya mambo ya kikubwa. Hapo awali inasemekana tatizo hili lilisababishwa na sababu za kisaikolojia pamoja na uzee au umri mkubwa ambapo viungo vya mwili vinakuwa vimechoka.
Kwa miaka ya hivi karibuni imebainika kuwa sababu zinazosababisha upungufu wa nguvu za kiume zimeongezeka na zifuatazo ni baadhi ya sababu hizo, nazo ni;
  • Kutokana na mabadiliko ya kisayansi na kukua kwa teknolojia wanaume wengi wamekuwa wakiishi maisha rahisi ya kutotumia miili yao kwa kufanya kazi zinazotumia nguvu na matokeo yake mwili unashindwa kujenga misuli imara katika viungo mbalimbali vya mwili.
  • Ulaji wa vyakula vilivyopitia viwandani na vyenye asili ya mafuta na protini nyingi ambapo vyakula hivyo vinakosa virutubisho muhimu kwa ajili ya kuimarisha viungo nyeti. Vyakula vyenye asili ya mafuta vinasababisha kuwepo kwa cholestral kwenye damu ambayo inapunguza au kuzuia mzunguko wa damu kwenye nyeti za mwanaume na hatimaye kushindwa kufanya kazi vizuri.
  • Matumizi ya mara kwa mara ya vileo/pombe, kahawa, uvutaji wa sigara nayo yanachangia upungufu wa nguvu za kiume.
  • Athari za magonjwa kama kisukari, arteri, magonjwa ya neva yanayosababishwa na ulaji wa vyakula vyenye protini nyingi na mafuta mengi.
  • Ukosefu wa madini na vitamini mbalimbali zinazopatikana kwa wingi kutoka kwenye matunda na mbogamboga.

Kutokana na kero ya tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au uhanithi, watu wengi wamekuwa wakijaribu kutumia vidonge ili waweze kuongeza nguvu na kufurahia tendo la ndoa. Imebainika kuwa matumizi ya vidonge hivyo yana madhara kwa afya ya mtumiaji. Baadhi ya athari anazoweza kuzipata mtumiaji wa dawa hizo ni pamoja na kuharisha, kichefuchefu, kuumwa na kichwa, kupooza baadhi ya viungo, upofu, kutosikia, na hata kupoteza kabisa kwa nguvu za kiume. Hali hiyo imewafanya watu wengi siku hizi wageukie matumizi ya dawa za mimea asilia au vyakula asilia ambapo havina athari kwa mtumiaji.

Hivyo basi mtu mwenye tatizo la uhanithi au upungufu wa nguvu za kiume anapaswa kuzingatia yafuatayo:

  • Kutumia kwa wingi matunda ikiwa kama sehemu ya mlo wake kila wakati anapopata mlo kwa siku tano hadi saba za mwanzo. Mtumiaji anaweza kuwa na milo mitatu kwa siku ambapo pia matumizi ya juisi ya zabibu, machungwa, apple, peas, nanasi, parachichi na tikitiki maji yanahimizwa.
  • Matumizi ya vyakula vya nafaka pia yanafufua matumaini kwa mtu aliyepoteza uweza wa kufanya tendo la ndoa kuweza kusimama upya. Inashauriwa pia mtumiaji atumie asali, mtindi, kitunguu saumu, mbogamboga na matunda mara kwa mara. Wakati huo huo mgonjwa aepuke matumizi ya sigara, pombe au vileo, kahawa, na vyakula vilivyopitia viwandani na vyenye protini na mafuta mengi.
  • Mazoezi ya viungo au mwili ama kufanya kazi zinazotumia nguvu nako kunasaidia kuimarisha viungo vya mwili. Iwapo mgonjwa atafanya kazi ya kutumia nguvu au mazoezi ya viungo japo dakika 30 hadi 45 kila siku na kisha kula vyakula vilivyoelezewa hapo juu anaweza kuwa na uwezo wa kusimama mwenyewe pasipo kutumia msaada wa vidonge vya kuongeza nguvu.

Pamoja na hayo machache mada ijayo nitaendeleza kutaja baadhi ya vyakula, matunda na matumizi ya mbogamboga na kazi zake katika kufufua uwezo wa wanaume aliyepoteza nguvu za kiume.

KILA LA KHERI.

2Flag.

1 comment:

Anonymous said...

Choose Generic Viagra and boost your sex-life into the orbit!!! Thanks for the great blog . I really enjoyed reading, I am a 68 year old man and I had problems of erectile dysfunction but it already was a stage closed in my life. I not want to go to the drugstore because made giving myself but I find the solution I Buy Viagra. The soft tabs are based on the same active ingredient as other erectile dysfunction pills: sildenafil citrate. Generic online pharmacy, no prescription needed is the most convenient place for you to buy cheap generic viagra order online and other quality prescription meds without prescription. I get exactly what I am looking for: top quality drugs, lowest prices, fast shipping and guaranteed satisfaction!